Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza
Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the love

Waziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya serikali ya nchi hiyo kuchapisha sheria kuhusu mkataba wenye utata na Rwanda wa kutuma wahamiaji katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Waziri wa Mambo ya Ndani, James Cleverly aliwaambia wabunge jana Jumatano kwamba Robert Jenrick amejiuzulu kwa madai kuwa sheria hiyo ya dharura haijitoshelezi.

“ Sikubaliani na sheria inayopendekezwa kwa sasa kupitia Bunge, kwani siamini kwamba inatupa fursa nzuri zaidi ya kufanikiwa,” ameandika waziri huyo katika barua aliyoielekeza kwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak.

Mapema Jumatano Rwanda ilionya kujiondoa katika mkataba wa kuwapokea wahamiaji iwapo Uingereza haitaheshimu sheria za kimataifa.

Uingereza na Rwanda zilitia saini mkataba mpya Jumanne katika jitihada za kufufua pendekezo linaloonekana kuwa na utata la Uingereza la kuwahamisha wahamiaji katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, pendekezo ambalo awali lilipingwa na mahakama ya Uingereza.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uingereza James Cleverly na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Vincent Biruta walitia saini makubaliano hayo mjini Kigali nchini Rwanda.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Vincent Biruta, ambaye alitia saini mkataba huo wa pande mbili, alisema ukiukaji wowote wa mikataba ya kimataifa unaweza kuifanya Rwanda kujiondoa katika mkataba huo.

Mpango wa Rwanda ni sehemu ya mkakati wa kupunguza idadi ya watu wanaoingia nchini Uingereza kwa kuvuka bahari kwa boti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!