Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serukamba aagiza kaya Singida kujenga vyoo bora kudhibiti kipindupindu
Afya

Serukamba aagiza kaya Singida kujenga vyoo bora kudhibiti kipindupindu

Spread the love

Mkuu wa  mkoa wa Singida, Peter Serukamba amewaagiza viongozi na watendaji mkoani humo kuhakikisha kaya zote zinakuwa na vyoo bora na kuchukua hatua kali kwa mujibu wa sheria dhidi ya kaya ambazo hazina vyoo ili kukabiliana na ugonjwa wa mlipuko wa kuhara na kipindupindu. Anaripoti Danson Kaijage, Singida… (endelea).

Akizungumza jana  Jumanne katika kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi cha mkoa, Serukamba amesema maradhi hayo husababishwa na mazingira ya uchafu.

Amesema jamii inapaswa kuhakikisha mazingira yote yanayowazunguka yanakuwa safi kwa lengo la kudhibiti magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu ili kisiwepo kabisa Mkoani Singida.

Aidha, Serukamba amewasisitiza wakuu wa wilaya wote mkoani humo kuhakikisha maeneo yote ya kaya, taasisi za umma, mashirika ya dini, masoko, stendi za mabasi, mashuleni, kwenye nyumba za ibada na mikusanyiko rasmi na isiyo rasmi, kutumia vifaa vya kunawia mikono, maji safi na sabuni ili kujikinga na maradhi hayo.

Amewasisitiza Wakuu hao wa Wilaya kwa kushirikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha maeneo yote ya kupikia na kuuzia vyakula yanakaguliwa na wataalamu wa Afya ili kuwa safi muda wote.

Peter Serukamba

Hata hivyo, Serukamba amewaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (SUWASA), Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Mkoa Singida (RUWASA) pamoja na Mkurugenzi wa Bodi Bonde la Kati kuhakikisha wanachukuwa sampuli za maji na kutibu visima vifupi, virefu na kusambaza maji safi na salama kwa watumiaji maji hayo ili kujikinga na ugonjwa huo wa kuharisha na kutapika.

Katika hatua nyingine, amewahimiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kuhakikisha maeneo yote ya minada na masoko yanakuwa na vyoo bora ili kuepuka kusambaa kwa ugonjwa huo wa mlipuko wa kuharisha na kutapika hasa katika Mkoa wa Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Afya

Mbunge ataka huduma Ultrasound itolewe bure kwa wajawazito

Spread the loveMBUNGE wa Viti Maalum, Esther Malleko, ameitaka Serikali kutoa bure...

Afya

Vituo 13 vyasitishiwa mkataba madai kutaka kupiga bilioni 4 za NHIF

Spread the loveVITUO vya kutoa huduma za afya 13, vimesitishiwa mikataba ya...

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

error: Content is protected !!