Monday , 13 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Viongozi wa Hamas wauawa, vifo vyafikia 3,785.
KimataifaTangulizi

Viongozi wa Hamas wauawa, vifo vyafikia 3,785.

Spread the love

TANGU vita baina ya taifa la Israel na wanamgambo wa Hamas kutoka Ukanda wa Gaza nchini Palestina viibuke tarehe 7 Okotoba 2023, kumeripotiwa mkururo wa vifo vya viongozi wa kundi hilo linalotajwa kuwa la kigaidi.

Vyombo vya habari vinavyohusiana na Hamas vimesema kuwa mkuu wa vikosi vya usalama vya Hamas ameuawa huko Gaza.

Watu wa familia ya Jehad Mheisen pia wanaripotiwa kufariki. Mjane wa mwanzilishi mwenza wa Hamas, Abdel Aziz al-Rantisi pia anaripotiwa kuuawa usiku wa kuamkia jana.

Aidha, Jeshi la Israel limesema ndege zake za kivita zilishambulia maeneo zaidi ya 100 na kumuua mwanachama mmoja wa Hamas ambaye inaaminika huenda alishiriki katika uvamizi huo wa tarehe 7 Oktoba  uliosababisha vifo vya watu 1,400 nchini Israel.

Hizo takwimu za hivi punde zaidi za wanachama wa Hamas waliofariki katika kile Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekitaja kuwa ni vita vya muda mrefu ambavyo nchi yake inaendesha dhidi ya Hamas.

Siku ya Jumatano, shirika la habari la AFP liliripoti kuwa Jamila Al-Shantee, mwanamke wa kwanza kuchaguliwa katika uongozi wa kisiasa wa Hamas aliuawa katika shambulio la Israel.

Mapema wiki hii, Vikosi vya Ulinzi vya Israel vilisema katika chapisho kwenye X, zamani Twitter, kwamba Ayman Nofal, aliyetajwa kama “afisa mkuu wa Hamas”, pia aliuawa.

Hayo yanajiri wakati Israel ikiendeleza mashambulizi dhidi ya kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza na hadi sasa idadi ya vifo inadaiwa kufikia watu 3,785.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Potofu huzaa potoshi/ potoshi huzaa potofu?

Spread the loveDayosisi 7 za KKKT katika kanda ya Ziwa na Magharibi,...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

error: Content is protected !!