Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Viongozi wa Hamas wauawa, vifo vyafikia 3,785.
KimataifaTangulizi

Viongozi wa Hamas wauawa, vifo vyafikia 3,785.

Spread the love

TANGU vita baina ya taifa la Israel na wanamgambo wa Hamas kutoka Ukanda wa Gaza nchini Palestina viibuke tarehe 7 Okotoba 2023, kumeripotiwa mkururo wa vifo vya viongozi wa kundi hilo linalotajwa kuwa la kigaidi.

Vyombo vya habari vinavyohusiana na Hamas vimesema kuwa mkuu wa vikosi vya usalama vya Hamas ameuawa huko Gaza.

Watu wa familia ya Jehad Mheisen pia wanaripotiwa kufariki. Mjane wa mwanzilishi mwenza wa Hamas, Abdel Aziz al-Rantisi pia anaripotiwa kuuawa usiku wa kuamkia jana.

Aidha, Jeshi la Israel limesema ndege zake za kivita zilishambulia maeneo zaidi ya 100 na kumuua mwanachama mmoja wa Hamas ambaye inaaminika huenda alishiriki katika uvamizi huo wa tarehe 7 Oktoba  uliosababisha vifo vya watu 1,400 nchini Israel.

Hizo takwimu za hivi punde zaidi za wanachama wa Hamas waliofariki katika kile Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekitaja kuwa ni vita vya muda mrefu ambavyo nchi yake inaendesha dhidi ya Hamas.

Siku ya Jumatano, shirika la habari la AFP liliripoti kuwa Jamila Al-Shantee, mwanamke wa kwanza kuchaguliwa katika uongozi wa kisiasa wa Hamas aliuawa katika shambulio la Israel.

Mapema wiki hii, Vikosi vya Ulinzi vya Israel vilisema katika chapisho kwenye X, zamani Twitter, kwamba Ayman Nofal, aliyetajwa kama “afisa mkuu wa Hamas”, pia aliuawa.

Hayo yanajiri wakati Israel ikiendeleza mashambulizi dhidi ya kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza na hadi sasa idadi ya vifo inadaiwa kufikia watu 3,785.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!