Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia aonya chuki, makundi Uchaguzi Serikali za mitaa
Habari za SiasaTangulizi

Samia aonya chuki, makundi Uchaguzi Serikali za mitaa

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania wadumishe amani na upendo kuelekea kipindi cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Rais Samia ametoa wito huo leo tarehe 16 Oktoba 2023, wakati akifungua Daraja la Msingi, lililoko wilayani Mkalama, Mkoa wa Singida.

“Niwaombe kuendelea kutunza amani na utulivu ndani ya nchi yetu, tunaelekea kwenye chaguzi mwakani,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amewataka wananchi kuepusha makundi kuelekea chaguzi zijazo “tujitahidi kuepusha makundi, najua kwenye uchaguzi pia una mkono wa Mungu inawezekana unataka sana kuchukua hiyo nafasi lakini Mungu hakukupangia kuchukua hiyo nafasi.”

“Kwa hiyo unapokosa tusianze kutengeneza makundi tukaanza kubomoa chama chetu tukafanya maendeleo yasipatikane tukaanza kufanya chuki, hapana huko tusifikie niwaombe sana dumisheni umoja wenu upendo na mshikamano tufanye chaguzi zetu vizuri zitupe sura chaguzi unaofuata,”amesema Rais Samia.

Mkuu huyo wa nchi amewataka wananchi kuwachagua viongozi watakaowatumikia.

“Tutakuwa na chaguzi za serikali za mitaa, niwaombe sana ndugu zangu kwenye jambo hili moja kuweka watu watakaowatumikia, msiende kuweka kwa watu watakaopitisha watu wengine, kama mnachagua watu katika uchaguzi ule wekeni watu ambao mnajua watakuja watutumikie wa Mkarama,”amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!