Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Muhongo ampa tano Rais Samia
Habari za Siasa

Prof. Muhongo ampa tano Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameipongeza Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha kiasi cha Sh. 4.75 bilioni, kwa ajili ya usambazaji maji katika kata mbili zilizokuwa zimeachwa katika mradi wa Maji ya Boma la Mugango-Kiabakari-Butiama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Pongezi hizo zimetolewa na tarehe 6 Aprili 2023 na Prof. Muhongo, kupitia taarifa iliyotolewa na Ofisi yake ya Jimbo la Musoma Vijijini.

“Tunaanza kwa kutoa shukrani nyingi sana kwa Serikali yetu inayoongozwa vizuri na Rais wetu, Dk. Samia. Kata mbili zilizokuwa zimeachwa kwenye mradi wa Sh. 71.5 bilioni wa maji sasa zimepatiwa fedha za kujengewa miundombinu ya usambazaji wa maji kwenye kata hizo , hii ni zawadi ya Pasaka,” imesema taarifa hiyo.

Kupitia taarifa hiyo, Prof. Muhongo amesema wananchi waishio kwenye chanzo cha maji katika Kata ya Mugango na Tegeruka, watapata maji kupitia bomba hilo.

“Mkandarasi wa mradi huu wa kata mbili ameshapatikana na taratibu zote zimekamilika, kifuatacho ni utiaji saini, hafla itakayofanyika kijijini Mayani, Kata ya Tegeruka, tarehe 12 Aprili 2023. Viongozi mbalimbali wa chama na Serikali watakuwepo,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!