Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA
Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the love

ALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald Kusaya ameteuliwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari hii leo tarehe 16 Machi 2023 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imeeleza kuwa Rais Samia pia amemteua Ally Gugu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma.

Gerald Kusaya aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa wa Rukwa.

Kabla ya uteuzi huo, Gugu alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara huku Tixon Nzunda akiteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, akichukua nafasi ya Willy Machumu ambaye amestaafu.

Aidha, Rais amemhamisha Fatuma Manga kutoka Mkoa wa Dodoma kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Singida, akichukua nafasi ya Dorothy Mwaluko ambaye amestaafu.

Rashid Mchata ametolewa Mkoa wa Rukwa kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Pwani akichukua nafasi ya Zuwena Jiri ambaye amehamishiwa Mkoa wa Lindi akichukua nafasi ya Ngussa Samike aliyepangiwa kazi nyingine.

1 Comment

  • CANADA Embassy and TACAIDS Here by requesting Trillion USD 56 to finance spread of diseases like HIV, Gonorea and Hapetititis B

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!