Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo Chadema kubanwa na kina Mdee mahakamani leo
Habari za Siasa

Vigogo Chadema kubanwa na kina Mdee mahakamani leo

Spread the love

 

WAJUMBE wa Bodi ya Wadhamini ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Azavel Lwaitama na Ruth Mollel, wanaanza kuhojiwa na mawakili wa wabunge viti maalum 19, katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu , jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ni katika kesi Na. 36/2022 iliyofunguliwa na wabunge hao wakiongozwa na Halima Mdee, kupinga uamuzi wa Chadema kuwavua uanachama kwa madai kuwa haikuwa halali, ambapo wanaiomba mahakama hiyo ifanye mapitio dhidi ya mchakato uliotumika katika suala hilo.

Leo tarehe 9 Machi 2023, Dk. Lwaitama na Mollel, wataanza kuhojiwa na mawakili wa kina Mdee, wakiongozwa na Wakili Ipilinga Panya, mbele ya Jaji Cyprian Mkeha.

Vigogo hao wa Chadema, wanatarajiwa kuhojiwa kuhusu hati zao kinzani, walizowasilisha mahakamani hapo kujibu malalamiko ya wabunge hao kwamba walifukuzwa Chadema kinyume cha Sheria.

Hatua hiyo inajiri baada ya Jaji Mkeha, Jumatatu iliyopita kuwapa ruhusa wabunge hao kuwahoji maswali ya dodoso wajumbe sita wa Bodi ya Wadhamini ya Chadema, ambapo mbali na Dk. Lwaitama na Mollel, wapo Mary Joackim, Francis Mushi, Maulidah Anna Komu na Ahmed Rashid Hamis.

Mawakili wa Mdee na wenzake, waliomba kuwahoji vigogo hao baada ya mawakili wa Chadema, wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala, kuwahoji maswali ya dodoso wabunge watano kati ya nane waliyopanga kuwauliza kuhusu malalamiko yao ya kufukuzwa na chama hicho.

Miongoni mwa wabunge waliohojiwa ni, Nusrat Hanje, Hawa Mwaifunga, Grace Tendega na Jesca Kishoa.

Chadema kupitia mawakili wao, waliiomba mahakama hiyo iache kuwahoji wabunge wengine watatu, Mdee, Ester Bulaya na Esther Matiko, kwa madai kuwa wametosheka na majibu yaliyotolewa na wenzao.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online kwa taarifa zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!