Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa achefukwa baba aliyemlawiti mwanaye, aagiza kukamatwa, MaRC, RPC kikaangoni
Habari Mchanganyiko

Majaliwa achefukwa baba aliyemlawiti mwanaye, aagiza kukamatwa, MaRC, RPC kikaangoni

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo wahakikishe wanamfikisha katika vyombo vya sheria baba mzazi wa mwanafunzi wa darasa la pili katika Kata ya Sokoni One mtaa wa Lonovono Jijini Arusha kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wake. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea)

Pia, amekemea vikali vitendo vya unyanyasaji, ubakaji na ulawiti kwa watoto na kuwataka Wakuu wa mikoa na makamanda wa polisi nchini wahakikishe wanawasaka na kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo viovu.

Majaliwa ametoa agizo hilo leo tarehe 17 Februari 2023 mkoani Songwe baada ya kusambaa kwa taarifa kupitia vyombo vya habari vikimuonesha mtoto huyo ambaye anadaiwa kulawitiwa na baba yake mzazi. Mtoto huyo ambaye alisikika akielezea namna mzazi wake huyo alivyokuwa akimfanyia vitendo vya ukatili.

Waziri Mkuu ameagiza mwanafunzi huyo pia naye atafutwe na kupatiwa huduma ya matibabu kwa haraka.

Amesema katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya baadhi ya wazazi,walezi na wanajamii kuwafanyia watoto vitendo vya ukatili ikiwemo ulawiti, hivyo kuwasababishia maumivu makali pamoja na msongo wa mawazo hali inayowafanya baadhi yao kushindwa kuendelea na masomo.

“Serikali haitosita kumchukulia hatua mzazi au mtu yeyote atakayebainika kufanya vitendo hivi vya ukatili.

“Kumeibuka wimbi la ukatili wa kuwafanyia vitendo vya hovyo watoto wetu kwenye maeneo mbalimbali nchini, hivyo fanyeni uchunguzi na kubaini wanaohusika na vitendo hivyo.

“Wakuu wa Mikoa, Makamanda wa Polisi pamoja na Maafisa wa Ustawi wa Jamii hakikisheni mnawasaka watu wote wenye tabia hizo na kuwachukulia hatua.”

Aidha, Majaliwa ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa jamii ishirikiane na Serikali katika kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto na wanawake.

“Wananchi shirikianeni kuhakikisha watoto wote wanalindwa na kupatiwa haki zao za msingi, mtoto wa mwenzio ni wako.”

Amesema baadhi ya wazazi wanadhani mtoto akipelekwa shule mwenye jukumu la kumuangalia mtoto ni mwalimu pekee huku wao wakiendelea na mambo mengine ya uzalishajimali ilihali watoto wakiendelea kuharibika hasa wanaolala kwenye mabweni.

Ameongeza kuwa kumeibuka sintofahamu kwa baadhi ya taasisi hizo kufundisha watoto ambao yasiyo ya kimaadili watoto wamekuwa wakifundishwa pia kubusiana na hata mambo machafu hivyo kuna kila sababu ya wakaguzi wa shule kuvikagua vitabu na kila shule itumia vitabu vilivyoainishwa na serikali.

“Nimepita halmashauri ya Songwe,Momba na hapa nipo Tunduma, maagizo haya nimetoa katika halmashauri zote vitabu ambavyo havitakiwi viondolewe mashuleni vitolewe vitabu elekezi vya kiada na ziada,nafahamu vitabu vingi vimeingizwa mitandaoni mamlaka husika simamieni hili tuviokoe vizazi vijavyo,’’ amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!