Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa
Spread the love

 

SERIKALI imewaagiza maafisa elimu wa mikoa na wilaya kuratibu usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni, ili kuepusha vitendo vya walimu kutoa adhabu zinazoathiri wanafunzi, kinyume cha sheria na waraka namba 24 wa 2002, kuhusu muongozo wa utoaji adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 2 Februari 2023 na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa, akizungumzia vitendo vya baadhi ya walimu kutoa adhabu kali kwa wanafunzi wanaofanya makosa shuleni.

“Natambua sio kusudio la walimu kuwadhuru wanafunzi, tukubaliane udhaifu wa uratibu wa usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni. Nitoe wito kwa maafisa elimu mkoa na wilaya kuwakumbusha walimu wetu nchini kuzingatia muongozo wa utoaji adhabu shuleni chini ya kifungu cha 61 cha Sheria ya Elimu Sura 356, pamoja na kanuni zake,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa amesema kuwa, miongozo ya adhabu inasisitiza kwamba adhabu ya viboko itatolewa iwapo patatokea utovu wa nidhamu au kosa kubwa litakalofanywa ndani au nje ya shule na au itashusha heshima ya shule.

Katika hatua nyingine, Waziri Majaliwa amewataka wananchi kutosambaza video zinazoonyesha walimu wakitoa adhabu kwa wanafunzi ili kuzuia taharuki kwenye jamii, badala yake watu wanaotekeleza vitendo hivyo waripotiwe kwa mamlaka husika ili hatua zichukuliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!