Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa
Spread the love

 

SERIKALI imewaagiza maafisa elimu wa mikoa na wilaya kuratibu usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni, ili kuepusha vitendo vya walimu kutoa adhabu zinazoathiri wanafunzi, kinyume cha sheria na waraka namba 24 wa 2002, kuhusu muongozo wa utoaji adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 2 Februari 2023 na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa, akizungumzia vitendo vya baadhi ya walimu kutoa adhabu kali kwa wanafunzi wanaofanya makosa shuleni.

“Natambua sio kusudio la walimu kuwadhuru wanafunzi, tukubaliane udhaifu wa uratibu wa usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni. Nitoe wito kwa maafisa elimu mkoa na wilaya kuwakumbusha walimu wetu nchini kuzingatia muongozo wa utoaji adhabu shuleni chini ya kifungu cha 61 cha Sheria ya Elimu Sura 356, pamoja na kanuni zake,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa amesema kuwa, miongozo ya adhabu inasisitiza kwamba adhabu ya viboko itatolewa iwapo patatokea utovu wa nidhamu au kosa kubwa litakalofanywa ndani au nje ya shule na au itashusha heshima ya shule.

Katika hatua nyingine, Waziri Majaliwa amewataka wananchi kutosambaza video zinazoonyesha walimu wakitoa adhabu kwa wanafunzi ili kuzuia taharuki kwenye jamii, badala yake watu wanaotekeleza vitendo hivyo waripotiwe kwa mamlaka husika ili hatua zichukuliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!