Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni
Habari za SiasaTangulizi

Serikali yatoa tamko bungeni sakatala la viboko shuleni

Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa
Spread the love

 

SERIKALI imewaagiza maafisa elimu wa mikoa na wilaya kuratibu usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni, ili kuepusha vitendo vya walimu kutoa adhabu zinazoathiri wanafunzi, kinyume cha sheria na waraka namba 24 wa 2002, kuhusu muongozo wa utoaji adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 2 Februari 2023 na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa, akizungumzia vitendo vya baadhi ya walimu kutoa adhabu kali kwa wanafunzi wanaofanya makosa shuleni.

“Natambua sio kusudio la walimu kuwadhuru wanafunzi, tukubaliane udhaifu wa uratibu wa usimamizi wa adhabu ya viboko shuleni. Nitoe wito kwa maafisa elimu mkoa na wilaya kuwakumbusha walimu wetu nchini kuzingatia muongozo wa utoaji adhabu shuleni chini ya kifungu cha 61 cha Sheria ya Elimu Sura 356, pamoja na kanuni zake,” amesema Waziri Majaliwa.

Waziri Majaliwa amesema kuwa, miongozo ya adhabu inasisitiza kwamba adhabu ya viboko itatolewa iwapo patatokea utovu wa nidhamu au kosa kubwa litakalofanywa ndani au nje ya shule na au itashusha heshima ya shule.

Katika hatua nyingine, Waziri Majaliwa amewataka wananchi kutosambaza video zinazoonyesha walimu wakitoa adhabu kwa wanafunzi ili kuzuia taharuki kwenye jamii, badala yake watu wanaotekeleza vitendo hivyo waripotiwe kwa mamlaka husika ili hatua zichukuliwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!