Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB yaingia makubaliano na Serikali Zanzibar uhifadhi bustani ya Forodhani
Habari Mchanganyiko

NMB yaingia makubaliano na Serikali Zanzibar uhifadhi bustani ya Forodhani

Spread the love

BENKI ya NMB imeingia makubaliano na Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, chini ya usimamizi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuboresha bustani ya Forodhani. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chini ya makubaliano hayo, Benki ya NMB itasimamia na kuhakikisha uwepo wa huduma na suluhishi za kifedha, elimu za kifedha na mikopo kwa wafanyabiashara wa Forodhani.

Itaweka maeneo maalum ya polisi, kubadilishia nguo wapiga mbizi na NMB Wakala.

Itaboresha maeneo ya kupiga mbizi Forodhani, na kutoa maboya kwa wapigambizi kwa ajili ya usalama wao sambamba na kuboresha taa zilizopo eneo la Forodhani.

Makubaliano haya yametiwa saini na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, Mhandisi Ali Said na Afisa Mkuu wetu wa Wateja Binafsi na Biashara – Filbert Mponzi huku wakishuhudiwa na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Simai Mohamed Said na viongozi wengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!