Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB yaingia makubaliano na Serikali Zanzibar uhifadhi bustani ya Forodhani
Habari Mchanganyiko

NMB yaingia makubaliano na Serikali Zanzibar uhifadhi bustani ya Forodhani

Spread the love

BENKI ya NMB imeingia makubaliano na Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, chini ya usimamizi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuboresha bustani ya Forodhani. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chini ya makubaliano hayo, Benki ya NMB itasimamia na kuhakikisha uwepo wa huduma na suluhishi za kifedha, elimu za kifedha na mikopo kwa wafanyabiashara wa Forodhani.

Itaweka maeneo maalum ya polisi, kubadilishia nguo wapiga mbizi na NMB Wakala.

Itaboresha maeneo ya kupiga mbizi Forodhani, na kutoa maboya kwa wapigambizi kwa ajili ya usalama wao sambamba na kuboresha taa zilizopo eneo la Forodhani.

Makubaliano haya yametiwa saini na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, Mhandisi Ali Said na Afisa Mkuu wetu wa Wateja Binafsi na Biashara – Filbert Mponzi huku wakishuhudiwa na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Simai Mohamed Said na viongozi wengine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!