Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa  Maelfu wafariki dunia kwa UVIKO-19 China
Kimataifa

 Maelfu wafariki dunia kwa UVIKO-19 China

Spread the love

 

WATU karibu 60,000 wamefariki dunia nchini China kwa Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19), kati ya tarehe 8 Desemba 2022 hadi tarehe 12 Januari mwaka huu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 14 Januari 2023 na Mkuu wa Tume ya Kitaifa ya Afya China (NHC), Jiao Yahui, watu 5,503 walifariki dunia kwa kushindwa kupumua, huku 54,435 walipoteza maisha kutokana na kuwa na magonjwa mengine tofauti na UVIKO-19.

Mitandao ya kimataifa imeripoti kuwa, vifo hivyo vimeongezeka baada ya China kusitisha utekelezaji wa sera yake ya kutokomeza ugonjwa huo ulioibuka 2019.

Akitoa taarifa hiyo, Yahui amesema asilimia 90.1 ya watu waliopoteza maisha walikuwa na umri wa miaka 65.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Bunge kumuweka katibu mkuu wa EAC kikaangoni

Spread the loveAliyekuwa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk. Peter...

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

error: Content is protected !!