Thursday , 9 May 2024
Home Gazeti Habari Spika Dk. Tulia awataka majaji wanawake kutenda haki
HabariHabari Mchanganyiko

Spika Dk. Tulia awataka majaji wanawake kutenda haki

Spread the love

 

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amewataka Majaji wa Mahakama nchini kuzingatia weledi, kufuata misingi ya kisheria na kutenda haki katika kazi zao.

Dk. Tulia ameyasema hayo leo tarehe 16 Januari, 2023 wakati akifungua Mkutano wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA) uliofanyika Mkoani Tanga kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

Amesema kuwa ni muhimu kuelewa kuwa siku zote mafanikio yao yasipimwe kwenye hukumu na maamuzi mangapi yaliyoandikwa na kutolewa tu, idadi ya vikao vya kesi walivyohudhuria au idadi ya mizozo iliyomalizika bali ni kwa jinsi gani nafasi zao katika Mahakama na maamuzi yametoa tafsiri katika kuiwezesha jamii kuondokana na ubaguzi na ukatili dhidi ya wanawake.

“Ni wakati wa kusimama imara kuweza kutimiza majukumu yenu hata pale kwenye vikwazo na changamoto za kijamii, kiimani na kitamaduni.

“Tukifanya hivyo, bila shaka tutakuwa sehemu ya kumwaga tone la maji litakalosambaa na kuwa dimbwi baadaye mto, ziwa na kuenea katika bahari kubwa ya jamii, na hivyo kufanya mwanamke kutoonekana Mhanga bali kuonekana Shupavu, Mpambanaji na Kiongozi,” amesisitiza Dk. Tulia

Sambamba na hayo, Spika amesema kuwa Bunge lake lipo tayari kupokea maoni ya mabadiliko ya sheria zilizopitwa na wakati ili kuzifanyia maboresho kwa lengo la kuhakikisha haki za makundi mbalimbali katika jamii zinalindwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!