Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP apangua makamanda wa mikoa, Muslim apelekwa Makao Makuu
Habari Mchanganyiko

IGP apangua makamanda wa mikoa, Muslim apelekwa Makao Makuu

IGP, Camilius Wambura
Spread the love

 

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, amefanya mabadiliko madogo ya Makamnda wa Polisi wa Mikoa ambapo wengine wamehamishiwa makao makuu na wengine kuhamishwa mikoa mingine. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mabadiliko hayo yamemgusa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mororgoro, SACP Fortunatus Muslim ambaye amehamishiwa kitengo cha mipango makao makuu wa polisi Dododma na nafasi yake kuchukuiwa na ACP Alex Mukama ambaye alikuwa Kmanda wa Polisi Mkoa wa Songwe.

Pia IGP Wambura amemhamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, ACP Theopista Mallya kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe.

Aidha amemhamisha ACP Shadrack Masija ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu Namba Moja Mkoa wa Simiyu kwenda kuwa Kamada wa Polisi Mkoa wa Rukwa.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo Ijumaa tarehe 6 Januari, 2023 na Msemaji wa Jeshi la Polisi SACP David Misime.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!