MKUU wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, amefanya mabadiliko madogo ya Makamnda wa Polisi wa Mikoa ambapo wengine wamehamishiwa makao makuu na wengine kuhamishwa mikoa mingine. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mabadiliko hayo yamemgusa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mororgoro, SACP Fortunatus Muslim ambaye amehamishiwa kitengo cha mipango makao makuu wa polisi Dododma na nafasi yake kuchukuiwa na ACP Alex Mukama ambaye alikuwa Kmanda wa Polisi Mkoa wa Songwe.
Pia IGP Wambura amemhamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, ACP Theopista Mallya kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe.
Aidha amemhamisha ACP Shadrack Masija ambaye alikuwa Afisa Mnadhimu Namba Moja Mkoa wa Simiyu kwenda kuwa Kamada wa Polisi Mkoa wa Rukwa.
Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo Ijumaa tarehe 6 Januari, 2023 na Msemaji wa Jeshi la Polisi SACP David Misime.
Leave a comment