RAIS Samia Suluhu Hassan ameeleza kusikitishwa na kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI aliyefariki dunia leoJumamosi saa 3: 34 Asubuhi tarehe 31 Desemba 2022 akiwa na umri wa miaka 95.
Rais Samia amesema Baba Benedikto alijitoa maisha yake kutumia wengine. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Katika ujumbe wake alioutoa kupitia mtandao wa Twitter Dk. Samia ametuma salama za pole kwa Baba Mtakatifu Francisko na waumini wa Kanisa Katoliki na duniani kote.
“Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedict XVI, ambaye alijitoa maisha yake kutumikia wengine. Natuma salamu za pole kwa Baba Mtakatifu Francisko, waumini wa Kanisa Katoliki Tanzania na Duniani kote. Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi. Amina”.
Baba Benedikto amefikwa na umauti akiwa katika makazi yake kwenye Hosteli ya Mater Ecclesiae iliyoko kwenye Bustani za Vatican ambako alikuwa anaishi tangu mwaka 2013 alipong’atuka kutoka madarakani kutokana na sababu za umri kuwa mkubwa.
Alifanya maamuzi haya magumu, ili kutoa nafasi kwa kiongozi mwingine, aweze kulitumikia Kanisa la Kristo Yesu, kwa ari na moyo mkuu.
Leave a comment