Saturday , 11 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Samia amlilia Papa Benedikto XVI
Habari Mchanganyiko

Dk. Samia amlilia Papa Benedikto XVI

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameeleza kusikitishwa na kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI aliyefariki dunia leoJumamosi saa 3: 34 Asubuhi tarehe 31 Desemba 2022 akiwa na umri wa miaka 95.

Rais Samia amesema Baba Benedikto alijitoa maisha yake kutumia wengine. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika ujumbe wake alioutoa kupitia mtandao wa Twitter Dk. Samia ametuma salama za pole kwa Baba Mtakatifu Francisko na waumini wa Kanisa Katoliki na duniani kote.

“Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Baba Mtakatifu Mstaafu Benedict XVI, ambaye alijitoa maisha yake kutumikia wengine. Natuma salamu za pole kwa Baba Mtakatifu Francisko, waumini wa Kanisa Katoliki Tanzania na Duniani kote. Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi. Amina”.

Baba Benedikto amefikwa na umauti akiwa katika makazi yake kwenye Hosteli ya Mater Ecclesiae iliyoko kwenye Bustani za Vatican ambako alikuwa anaishi tangu mwaka 2013 alipong’atuka kutoka madarakani kutokana na sababu za umri kuwa mkubwa.

Alifanya maamuzi haya magumu, ili kutoa nafasi kwa kiongozi mwingine, aweze kulitumikia Kanisa la Kristo Yesu, kwa ari na moyo mkuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!