Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mazishi ya Papa Benedict XVI kufanyika Alhamisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Mazishi ya Papa Benedict XVI kufanyika Alhamisi

Spread the love

MAZISHI ya Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI aliyefariki dunia leoJumamosi saa 3: 34 Asubuhi tarehe 31 Desemba 2022 akiwa na umri wa miaka 95, yatafanyika Alhamis tarehe 5 Januari na yataongozwa na Papa Francis. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Baba Benedikto amefikwa na umauti akiwa katika makazi yake kwenye Hosteli ya Mater Ecclesiae iliyoko kwenye Bustani za Vatican ambako alikuwa anaishi tangu mwaka 2013 alipong’atuka kutoka madarakani kutokana na sababu za umri kuwa mkubwa.

Alifanya maamuzi haya magumu, ili kutoa nafasi kwa kiongozi mwingine, aweze kulitumikia Kanisa la Kristo Yesu, kwa ari na moyo mkuu.

Kwa mujibu wa Vatican News wamealikwa watu mbalimbali kuungana na Mama Kanisa kwa ajili ya kumwombea maisha ya uzima wa milele Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI.

Aidha, Kiongozi wa Ujerumani ametoa salamu za rambirambi kwa mjerumani mwenzake.

Kansela Olaf Scholz ametuma ujumbe wake kwenye mtandao wa Twitter akisema Papa huyo wa zamani alikuwa “kwa wengi, sio tu katika nchi hii, kiongozi maalum wa kanisa”, amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!