Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mazishi ya Papa Benedict XVI kufanyika Alhamisi
Habari MchanganyikoTangulizi

Mazishi ya Papa Benedict XVI kufanyika Alhamisi

Spread the love

MAZISHI ya Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI aliyefariki dunia leoJumamosi saa 3: 34 Asubuhi tarehe 31 Desemba 2022 akiwa na umri wa miaka 95, yatafanyika Alhamis tarehe 5 Januari na yataongozwa na Papa Francis. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Baba Benedikto amefikwa na umauti akiwa katika makazi yake kwenye Hosteli ya Mater Ecclesiae iliyoko kwenye Bustani za Vatican ambako alikuwa anaishi tangu mwaka 2013 alipong’atuka kutoka madarakani kutokana na sababu za umri kuwa mkubwa.

Alifanya maamuzi haya magumu, ili kutoa nafasi kwa kiongozi mwingine, aweze kulitumikia Kanisa la Kristo Yesu, kwa ari na moyo mkuu.

Kwa mujibu wa Vatican News wamealikwa watu mbalimbali kuungana na Mama Kanisa kwa ajili ya kumwombea maisha ya uzima wa milele Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI.

Aidha, Kiongozi wa Ujerumani ametoa salamu za rambirambi kwa mjerumani mwenzake.

Kansela Olaf Scholz ametuma ujumbe wake kwenye mtandao wa Twitter akisema Papa huyo wa zamani alikuwa “kwa wengi, sio tu katika nchi hii, kiongozi maalum wa kanisa”, amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

error: Content is protected !!