Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanajeshi 8 wahukumiwa kifo kwa mauaji ya Mchina
Kimataifa

Wanajeshi 8 wahukumiwa kifo kwa mauaji ya Mchina

Kitanzi
Spread the love

 

WANAJESHI nane na raia moja katika eneo la kaskazini mashariki mwa DRC lililogubikwa na vita, wamehukumiwa kifo kwa mauaji raia mmoja wa China na ubadhirifu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Wote walipatikana na hatia ya mauaji na kujihusisha na uhalifu wakiwemo kanali Mukalenga Tendeko na Kayumba Sumahili.

Wanajeshi wengine watatu ambao walikuwa wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela katika kesi hiyo, waliachiliwa huru.

Maafisa hao wawili wakuu walituhumiwa kupanga shambulio dhidi ya msafara uliokuwa umebeba dhahabu, pesa taslimu dola 6,000 na wafanyakazi raia wa China kupitia eneo la Irumu katika jimbo la Ituri nchini humo.

Msafara huo ambao ulikuwa unarejea kutoka mgodi wa dhahabu, ulishambuliwa tarehe 17 Machi mwaka huu kwenye kijiji cha Nderemi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!