WANAJESHI nane na raia moja katika eneo la kaskazini mashariki mwa DRC lililogubikwa na vita, wamehukumiwa kifo kwa mauaji raia mmoja wa China na ubadhirifu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Wote walipatikana na hatia ya mauaji na kujihusisha na uhalifu wakiwemo kanali Mukalenga Tendeko na Kayumba Sumahili.
Wanajeshi wengine watatu ambao walikuwa wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela katika kesi hiyo, waliachiliwa huru.
Maafisa hao wawili wakuu walituhumiwa kupanga shambulio dhidi ya msafara uliokuwa umebeba dhahabu, pesa taslimu dola 6,000 na wafanyakazi raia wa China kupitia eneo la Irumu katika jimbo la Ituri nchini humo.
Msafara huo ambao ulikuwa unarejea kutoka mgodi wa dhahabu, ulishambuliwa tarehe 17 Machi mwaka huu kwenye kijiji cha Nderemi.
Leave a comment