Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wasaidizi wa Samia matumbo joto, kupanguliwa wakati wowote
Habari za Siasa

Wasaidizi wa Samia matumbo joto, kupanguliwa wakati wowote

Spread the love

RAIS wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amesema amekusudia kufanya mabadiliko ya baadhi ya viongozi wa Serikali ili kuachana na viongozi ambao wanashindwa kuendana na kasi yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea). 

Dk Samia amesema hayo leo tarehe 8 Disemba 2022 katika Mkutano wa 10 wa chama hicho ambao leo umefikia tamatu mkoani Dodoma.

Amesema kuwa bado wanasafari ya miaka mitatu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2025, ili wananchi wawe mashuhuda wa yanayofanywa.

“Kubwa zaidi tunapokwenda kwa wananchi, ni wananchi wenyewe wanayosema serikali waliyofanya kwao, tofauti na utamaduni tuliokuwa nao nyuma, kwamba tunapokwenda kwa wananchi serikali ndio tunawaambiwa tumewafanyia, wakati mwingine wanashangaa hiki kimefanyika wapi,” amesema Dk. Samia.

Amesema mabadiliko hayo yatatoa nafasi kwa wananchi kuona na kutoa tathmini ya yaliyofanyika na wenyewe kuwa mashuhuda wa kila kinachofanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!