Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mdee, wenzake yapigwa kalenda hadi Machi 2023
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya Mdee, wenzake yapigwa kalenda hadi Machi 2023

Spread the love

 

KESI ya kupinga kuvuliwa uanachama wa Chama cha Chadema, iliyofunguliwa na wabunge viti maalum 19 katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu, jijini Dar es Salaam, imeahirishwa hadi Machi 2023, baada ya kiongozi wa Jopo la Mawakili wa chama hicho, Wakili Peter Kibatala, kupata dharura. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kesi hiyo imeahirishwa leo Jumanne, tarehe 6 Desemba 2022 na Mahakama hiyo mbele ya Jaji Cyprian Mkeha, baada ya mawakili wa Chadema kupitia Wakili Jeremiah Mtobesya kuomba ahirisho akidai Wakili Kibatala, yuko nje ya Dar es Salaam.

Wakili Mtobesya amedai kuwa, Wakili Kibatala yuko jijini Mwanza kwa ajili ya kusimamia kesi ya mauaji.

Kufuatia ombi hilo, mawakili wa wabunge viti maalum walilikubali kisha Jaji Mkeha akaahirisha kesi hadi Machi 2023 kuanzia tarehe 6 hadi 9.

Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya usikilizwaji ambapo mawakili wa Chadema walitarajia kumaliza kumhoji maswali ya dodoso Mbunge Viti Maalum, Jesca Kishoa, kuhusu malalamiko yake ya kufukuzwa Chadema bila kupewa nafasi ya kusikilizwa.

Kesi hiyo itakapokuja kusikilizwa Machi 2023, Kishoa ataendelea kuulizwa maswali ya dodoso na mawakili wa Chadema. Alianza kuhojiwa tarehe 9 Novemba 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!