Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Ihefu yavunja rekodi ya Yanga, yaipiga 2-1
MichezoTangulizi

Ihefu yavunja rekodi ya Yanga, yaipiga 2-1

Spread the love

 

WAKULIMA wa mpunga kutoka wilayani Mbarali mkoani Mbeya, Ihefu FC wameivunja rekodi ya Mabingwa wa Ligi Kuu Bara, Yanga SC. ya kutofungwa mechi 50 kuanzia msimu uliopita na msimu huu wa 2022/2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Yanga ambao walikuwa wageni mkoani Mbeya, walikuwa wakisherehekea kufikisha mechi 49 bila kufungwa na kujinafananisha na Klabu maarufu ya Arsenal inayoshiriki Ligi kuu Uingereza.

Hata hivyo, katika mtanange huo uliopigwa leo tarehe 29 Novemba, 2022, umewaduwaza mashabiki wa Yanga baada ya kukubali kichapo cha bao 2-1 kutoka kwa Ihefu ambao walikuwa wakiburuza mkia katika msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Licha ya Yanga kuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 9 ambalo lilitiwa kimyani Yannick Bangala, Ihefu walikuja kwa kasi na kufanikiwa kuandika bao la kwanza kupitia kwa Never Tigere dakika ya 39 na Lenny Kissu dakika ya 62.

Pamoja na Mwalimu wa Yanga, Nasreddine Nabi kufanya mabadiliko ya wachezaji hususani katika safu ya kiungo, bado timu ya Ihefu ilicheza kwa kujilinda katika dakika zote 90 na kujihakikishia ushindi.

Kwa matokeo hayo, Yanga imebaki kileleni na pointi 32 pamoja na mchezo mmoja mkononi wakati Azam wakifuatia kwa kufungana pinti na Yanga lakini wakizidiwa kwa uwiano wa magoli ya kufungwa na kufunga.

Ihefu waliokuwa wanaburuza mkia kwa pointi 8, sasa wamefikisha pointi 12 baada ya kushuka dimbani mara 14.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!