Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Mbarawa atembelea banda la TMA, aelezwa umuhimu wa taarifa za hali ya hewa
Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa atembelea banda la TMA, aelezwa umuhimu wa taarifa za hali ya hewa

Spread the love

 

WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa jana alitembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na kupata maelezo mbalimbali ikiwa pamoja na kuelezwa umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika misimu tofauti tofauti. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Waziri Mbarawa alitembelea banda hilo katika maonesho yaliyoandaliwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa lengo la kutangaza kazi za taasisi mbalimbali zilizopo chini ya wizara hiyo kupitia mkutano wa 15 wa wadau wa kutathmini utendaji kazi wa sekta ya uchukuzi kwa mwaka mmoja, uliofanyika katika ukumbi wa Kisenga LAPF – Dar es Salaam.

Prof. Mbarawa aliambatana na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Africa (AFDO) Dk. Patricia Laverley, pamoja na mambo mengine walielezwa umuhimu wa huduma za hali ya hewa kwa sekta ya ujenzi na uchukuzi ikiwa ni pamoja na huduma mahususi za usafiri wa barabara, maji na anga.

Aidha, kupitia maonesho hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Wilbert Muruke alielezea umuhimu wa huduma za hali ya hewa katika sekta ya uchukuzi jinsi zinavyosaidia katika kutekeleza majukumu ya sekta vilevile kukabiliana na athari zitokanazo na hali mbaya ya hewa.

“Kama mnavyoelewa huduma za hali ya hewa ni mtambuka kwa sekta mbalimbali mojawapo ya sekta ambayo tunaihudumia ni sekta ya usafirishaji ambapo katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo viwanja vya ndege, reli, barabara na madaraja moja ya taarifa muhimu katika mipango yao ni taarifa za hali ya hewa zitakazowawezesha kupanga vyema mipango yao na hivyo kusaidia kuepusha hasara zitakazojitokeza kutokana na majanga yatokanayo na hali mbaya ya hewa,” alisema Muruke.

Muruke aliongezea kwa kuwataka wadau kuendelea kufuatilia taarifa mbalimbali za hali ya hewa zinazotolewa mara kwa mara na TMA hususani katika kipindi hiki ambacho dunia imeendelea kukumbwa na mabadiliko ya hali ya hewa, kwani itasaidia kupunguza au kuepusha hasara zinazoweza kujitokeza kutokana na hali mbaya ya hewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!