Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mpango aagiza Ma-RC, DC kuwaondoa waliojenga kwenye vyanzo vya maji
Habari Mchanganyiko

Dk. Mpango aagiza Ma-RC, DC kuwaondoa waliojenga kwenye vyanzo vya maji

Spread the love

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango amewaagiza wakuu wilaya na mikoa kushirikiana na mamlaka zingine kuwaaondoa wananchi wote wanaoishi na kuendesha shughuli za uchumi kama vile kilimo na mifugo maeneo ya milima iliyopo karibu na vyanzo vya maji. Anaripoti Kenneth Ngelesi, Mbeya … (endelea).

Dk. Mpango ametoa agizo hilo mkoani Mbeya leo tarehe 16 Novemba, 2022 wakati wa akizindua kampeni ya kupanda miti rafiki na vyanzo vya maji lililofanyika katika chanzo cha maji cha Nzovwe jijini Mbeya ambapo miti milioni mbili inatarajiwa kupandwa.

Aidha, ameiagiza wakala wa huduma za misitu nchini TFS kuhakikisha wanatambua miti rafiki na maji kulingana na eneo husika ikiwa ni pamoja na kuandaa vitalu na miche ya kutosha na kuipanda katika vyanzo vya maji kwenye mikoa yote badala ya kuwa na miti ya kibiashara pekee.

Wakati huo huo Dk. Mpango amefungua mkutano mkuu wa nane wa mwaka wa bodi za maji za mabonde uliofanyika mkoani Mbeya na kuwaagiza wadau wa mazingira wa kiwemo NEMC kuacha kutoa vibali vya kufanya shughuli za kiuchumi kwenye maeneo ya vyanzo vya maji.

Wakati Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amesema ni vema TFS kupanda miti ya asili badala ya miti ya kibiashara ambayo ikifiki wakati wa kuvuna eneo linakiuwa wazi.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Maji Juma Aweso, Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano, Dk. Sulemani Jaffo, wakuu wa mikoa kutoka mikoa ya Nyanda za Juu kusini pamoja na wakuu wa taasisi za kisekta na Wakurugenzi watendaji wa mabonde yote tisa nchini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!