Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanawake Ubungo waandamana hadi kwa DC kudai maji
Habari Mchanganyiko

Wanawake Ubungo waandamana hadi kwa DC kudai maji

Spread the love

WANAWAKE kadhaa wa Kata ya Luguruni wameandamana hadi ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Herry James, wakidai kutopata huduma ya maji kwa miezi mitatu sasa. Anaripoti Mwandishi Wetu Dar es Salaam … (endelea)

Akina mama hao wameandamana wakiwa na ndoo tupu kichani huku wakiimba nyimbo za wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti kuwatua ndoo hizo kichwani.

Mara baada ya kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita, Rais Samia aliahidi kuwatua akina mama ndoo kichwani na kuongeza bajeti ya maji karibu mara mbili ili kufanikisha azma hiyo.

Kheri James, Mkuu wilaya ya Ubungo

Hata hivyo kutokana na ukame ulio yakumba maeneo mengi ya nchi, mito inayotegemewa kuzalisha maji imekauka na kusababisha uhaba mkubwa wa maji.

Mkuu wa Wilaya hiyo James, amewahakikishia wanawake hao kuwa maji yatatoka hii leo kufikia majira ya saa 7 na kuziagiza mamalak za maji kuzingatia ratiba ya mgawo wa maji.

Ameonya kuwa wananchi wanakosa maji ilihali maeneo mengine maji yanamwagika barabarani kutokana na ubovu wa miundombinu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!