WANAWAKE kadhaa wa Kata ya Luguruni wameandamana hadi ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Herry James, wakidai kutopata huduma ya maji kwa miezi mitatu sasa. Anaripoti Mwandishi Wetu Dar es Salaam … (endelea)
Akina mama hao wameandamana wakiwa na ndoo tupu kichani huku wakiimba nyimbo za wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Wilaya na Mwenyekiti kuwatua ndoo hizo kichwani.
Mara baada ya kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita, Rais Samia aliahidi kuwatua akina mama ndoo kichwani na kuongeza bajeti ya maji karibu mara mbili ili kufanikisha azma hiyo.
Hata hivyo kutokana na ukame ulio yakumba maeneo mengi ya nchi, mito inayotegemewa kuzalisha maji imekauka na kusababisha uhaba mkubwa wa maji.
Mkuu wa Wilaya hiyo James, amewahakikishia wanawake hao kuwa maji yatatoka hii leo kufikia majira ya saa 7 na kuziagiza mamalak za maji kuzingatia ratiba ya mgawo wa maji.
Ameonya kuwa wananchi wanakosa maji ilihali maeneo mengine maji yanamwagika barabarani kutokana na ubovu wa miundombinu.
Leave a comment