Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Idadi watu waliokuwemo ndani ya ndege yazua utata, mmoja atimua mbio
Habari Mchanganyiko

Idadi watu waliokuwemo ndani ya ndege yazua utata, mmoja atimua mbio

Baadhi ya abiria waliokolewa katika ajali ya ndege ya Precision
Spread the love

 

WAKATI taarifa rasmi za idadi ya watu waliokuwemo ndani ya ndege ya Precision Air iliyopata ajali leo Jumapili katika Ziwa Victoria mkoani Kagera ikitajwa kuwa ni 43, imebainika kuwa jumla ya watu waliokuwemo ndani ya ndege hiyo ni 45 wakiwamo marubani na wahudumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Bukoba … (endelea).

Hatua hiyo imekuja wakati taarifa ya Jeshi la Polisi pamoja na Kampuni hiyo ya Precision Air zikibainisha kuwa abiria walikuwa 39 akiwamo mtoto mmoja na wafanyakazi wanne.

Hata hivyo, katika taarifa iliyotolewa jioni tarehe 6 Novemba, 2022 na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila imebainisha kuwa ndege hiyo ilikuwa na idadi ya watu 45.

Amesema wakati wa uokozi imebainika kulikuwa na jumla ya abiria 41 na wahudumu wanne.

“Jumla ya watu 19 wamefariki dunia wakiwemo rubani na msaidizi wake. Aidha waliookolewa ni watu 26 kati yao mmoja baada ya kuokolewa alikimbia na hajulikani alikokwenda,” imesema taarifa hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila

Ndege hiyi iliyokuwa inatokea Dar es Salaam kuelekea Mwanza kupitia Bukoba, ilishindwa kutua katika Uwanja wa Bukoba na kulazimika kutua ziwani.

Aidha, taarifa za awali zinaeleza kuwa chanzo cha ajali ya ndege hiyo yenye usajili namba 5H-PWF, ni hali mbaya ya hewa hasa upepo ndio uliosababisha rubani ashindwe kutua katika uwanja wa kutua mita takribani 100 ndani ya maji kutoka ziwani.

Chalamila amesema zoezi ka uokoaji limeendeshwa kwa ushirikiano na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na jioni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alishitiki zoezi hiko pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

Habari Mchanganyiko

Bil 12.4 zimetumika ujenzi wa miradi wilaya ya Momba

Spread the love MKUU wa wilaya ya Momba mkoani Songwe Kennan Kihongosi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

error: Content is protected !!