Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bwege aalikwa kumpigia kampeni Raila Odinga
Habari MchanganyikoTangulizi

Bwege aalikwa kumpigia kampeni Raila Odinga

Spread the love

MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini Selemani Said Bungara (Bwege) amealikwa nchini Kenya kumpigia kampeni mgombea wa Azimio la Umoja, Raila Odinga. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 4 Agosti, 2022 na Janeth Rithe, Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo.

Bwege ambaye mwaka 2020 aligombea ubunge kupitia Chama cha ACT-Wazalendo na kuangushwa na mpinzani wake wa Chama cha Mapinduzi, amewasili nchini humo kwa ndege Air Tanzania mapema leo.

“Bwege ndio Mwanasiasa wa kwanza kutoka Tanzania kupewa heshima hiyo na Timu ya Kampeni ya Azimio la Umoja,” ikiwa ni wiki ya lala salama kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika wiki ijayo tarehe 9 Agosti, 2022.

“Kumbukumbu za mtandaoni zinaonesha kuwa hotuba za Bwege ndani na nje ya Bunge zinafuatiliwa na kupendwa sana nchini Kenya,” amesema Rithe.

Mvuto wa Bwege kwa Wakenya wengi inaweza kutumika  kama karata ya mwisho kwenda kuongeza kura za Odinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

error: Content is protected !!