MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini Selemani Said Bungara (Bwege) amealikwa nchini Kenya kumpigia kampeni mgombea wa Azimio la Umoja, Raila Odinga. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 4 Agosti, 2022 na Janeth Rithe, Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo.
Bwege ambaye mwaka 2020 aligombea ubunge kupitia Chama cha ACT-Wazalendo na kuangushwa na mpinzani wake wa Chama cha Mapinduzi, amewasili nchini humo kwa ndege Air Tanzania mapema leo.
“Bwege ndio Mwanasiasa wa kwanza kutoka Tanzania kupewa heshima hiyo na Timu ya Kampeni ya Azimio la Umoja,” ikiwa ni wiki ya lala salama kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika wiki ijayo tarehe 9 Agosti, 2022.
“Kumbukumbu za mtandaoni zinaonesha kuwa hotuba za Bwege ndani na nje ya Bunge zinafuatiliwa na kupendwa sana nchini Kenya,” amesema Rithe.
Mvuto wa Bwege kwa Wakenya wengi inaweza kutumika kama karata ya mwisho kwenda kuongeza kura za Odinga.
Leave a comment