Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mgombea Kenya asafisha vyoo kushawishi wapiga kura
Kimataifa

Mgombea Kenya asafisha vyoo kushawishi wapiga kura

Spread the love

 

KUELEKEA Uchaguzi wa Kenya unaotarajiwa kufanyika Agosti 9, 2022 imezuka mishangao kwa wananchi mara baada ya baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi kuonekana wakitumia mbinu shawishi ili kuvutia wananchi hao kuwachagua. Anaripoti Erick Mbawala kwa msaada wa mashirika ya kimataifa … (endelea). 

Hii imedhihirika baada ya baadhi ya wagombea kuonekana wakijumuika katika shughuli za kawaida za kimaendeleo kwenye jamii ambazo hufanywa kila siku na wakazi wa maeneo husika kama vile kusafisha vyoo, kukata mbogamboga na kupika chai.

Moja kati ya wanasiasa ambaye ni mgombea wa kiti cha ugavana Nairobi, Polycarp Igathe, ameonekana amevaa ovaroli, buti na gravu kabla ya kuchukua ndoo yenye maji na kuanza kusafisha vyoo katika mji mkuu, Nairobi.

Pia Igathe amepigwa picha akiosha magari na kushiriki vinywaji katika vilabu vya burudani nyakati za usiku.

Watu wengi wameikejeli njia hiyo lakini Igathe ambaye ni mpinzani wa Seneta wa Nairobi, Johnson Sakaja, kwa upande wake ameona ni njia mojawapo ya uwajibikaji katika majukumu ya kulijenga taifa.

“Kwa muda mrefu imeonekana kama kazi chafu lakini hii ni kazi ya kuwajibika,” amesema Igathe.
Wachambuzi wa masuala ya siasa wametaja hatua hiyo kama mbinu ya kuwashawishi wananchi kumchagua kuelekea uchaguzi huo na pia wametaja kuwa ni kama namna ya kujenga uhusiano mwema baina yake na wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!