Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kiboko ‘babu’ aliyeua watu 8, auawa
Habari Mchanganyiko

Kiboko ‘babu’ aliyeua watu 8, auawa

Spread the love

KIBOKO dume ambaye kwa muda mrefu amekuwa akisumbua wananchi wa kata ya Mabilioni wilayani Same Mkoa wa Kilimanjaro na kukwamisha shughuli za maendeleo kama kilimo, ufugaji na uchotaji wa maji katika Mto Pangani, ameuawa kwa kupigwa risasi katika msako ulioongozwa na vikosi kutoka TAWA. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkuu wa Wilaya ya Same, Edward Mpogoro akizungumza baada ya kiboko Babu kuuawa.

Kiboko huyo aliyepewa jina la Babu ambaye ameua watu zaidi ya sita, ng’ombe 8, punda na mbuzi tangu mwaka 2017 alikuwa akihusishwa na imani za kishirikina kwani jitihada mbalimbali za kumdhibiti hazikufanikiwa katika kipindi chote

Tarehe 17 Juni 2022 kiboko huyo alimuua kwa kumshambulia mwanaume mmoja aliyekuwa anakwenda shambani kumwagilia ndipo Mkuu wa Wilaya ya Same, Edward Mpogolo alipoagiza kuhakikisha kila mbinu zinatumika kumuua kiboko huyo ili wananchi warudi kufanya shughuli za maendeleo kwa amani.

Baada ya kuanza msako kiboko huyo aliuawa tarehe 28 Julai 2022 saa 11 alfajiri baada ya kuweka mtego na kupigwa risasi ya kichwa na Mzee Ally Miraji Sengela (hunter) aliyesaidiwa na Mzee Fue Omary Ngerwa (Mvuvi na Mweka Mtego) kwa kushirikiana na wahifadhi wa TAWA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!