Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ataja mbinu kuinua kilimo Afrika Mashariki
Habari za Siasa

Rais Samia ataja mbinu kuinua kilimo Afrika Mashariki

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amezihimiza nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharik (EAC), kuboresha sekta ya kilimo, ili uzalishaji wa mazao uongezeke na kuondoa utegemezi wa chakula kutoka nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Rais Samia ametoa wito huo leo Alhamisi, tarehe 21 Julai 2022, katika mkutano wa kawaida wa 22 wa wakuu wa nchi za EAC, uliofanyika jijini Arusha, baada ya kuulizwa swali nini kifanyike ili nchi hizo ziweze kujilisha zenyewe.

Mkuu huyo wa Tanzania, amesema mageuzi hayo yanabidi yaende sambamba na utekelezaji wa miradi ya maji, ili kuimarisha kilimo cha umwagiliaji wakati wa ukame.

“Ardhi peke yake haitoshi, tunatakiwa tuangalie maji, namna ya kumwagilia ardhi. Miradi ya maji ni mizuri namna gani tutavuna maji ya mvua tupate maji tumwagilie mashamba. Suala lingine kuangalia namna ya kupata fedha na pembejeo za kisasa,” amesema Rais Samia.

https://youtu.be/qd_QI_q822E

Katika hatua nyingine, Rais Samia ameshauri wakulima wasaidiwe fedha, pamoja na kuwajengea uwezo wa kutunza mazao yao kabla na baada ya kuvuna.

“Vyanzo vya fedha, wakulima waweze kusaidiwa kubadilisha kilimo chetu Afrika Mashariki, lingine tunapoteza sana mazao kipindi cha mavuno na kabla ya mavuno ambapo mazao yako shambani. Kwa kweli baada ya kuvuna tunapoteza tunatakiwa tuwe na mbinu ya kuvuna mazao yetu,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!