Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ataja mbinu kuinua kilimo Afrika Mashariki
Habari za Siasa

Rais Samia ataja mbinu kuinua kilimo Afrika Mashariki

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amezihimiza nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharik (EAC), kuboresha sekta ya kilimo, ili uzalishaji wa mazao uongezeke na kuondoa utegemezi wa chakula kutoka nje. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Rais Samia ametoa wito huo leo Alhamisi, tarehe 21 Julai 2022, katika mkutano wa kawaida wa 22 wa wakuu wa nchi za EAC, uliofanyika jijini Arusha, baada ya kuulizwa swali nini kifanyike ili nchi hizo ziweze kujilisha zenyewe.

Mkuu huyo wa Tanzania, amesema mageuzi hayo yanabidi yaende sambamba na utekelezaji wa miradi ya maji, ili kuimarisha kilimo cha umwagiliaji wakati wa ukame.

“Ardhi peke yake haitoshi, tunatakiwa tuangalie maji, namna ya kumwagilia ardhi. Miradi ya maji ni mizuri namna gani tutavuna maji ya mvua tupate maji tumwagilie mashamba. Suala lingine kuangalia namna ya kupata fedha na pembejeo za kisasa,” amesema Rais Samia.

https://youtu.be/qd_QI_q822E

Katika hatua nyingine, Rais Samia ameshauri wakulima wasaidiwe fedha, pamoja na kuwajengea uwezo wa kutunza mazao yao kabla na baada ya kuvuna.

“Vyanzo vya fedha, wakulima waweze kusaidiwa kubadilisha kilimo chetu Afrika Mashariki, lingine tunapoteza sana mazao kipindi cha mavuno na kabla ya mavuno ambapo mazao yako shambani. Kwa kweli baada ya kuvuna tunapoteza tunatakiwa tuwe na mbinu ya kuvuna mazao yetu,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!