Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wadau wataka ushirikishwaji kamati kufumua vyombo vya dola
Habari za SiasaTangulizi

Wadau wataka ushirikishwaji kamati kufumua vyombo vya dola

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameshauriwa kushirikisha wadau katika uundaji wa kamati ya kushauri namna bora ya ufumuaji wa vyombo vya haki jinai nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo ulitolewa jana tarehe 20 Julai 2022, muda mfupi baada ya Rais Samia kusema ameunda kamati ya wajumbe 12 na sekretarieti yenye watu watano ikiongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Mohamed Chande Othman, kwa ajili ya kumshauri namna ya kuleta mabadiliko ya utendaji wa vyombo hivyo, vikiongozwa na Jeshi la Polisi.

Msemaji wa Sekta ya Mambo ya Ndani wa ACT-Wazalendo, Maharagande Mbarala, amesema kamati hiyo ni vyema ikashirikisha wadau wanaoguswa na huduma ya Jeshi la Polisi, ili kuleta matokeo chanya.

“Uamuzi wa Rais kuunda tume ya wastaafu wenye kushauri mageuzi ya Jeshi la Polisi ni muhimu iwe shirikishi zaidi, kwa kuwahusisha wadau wote wanaoguswa na huduma ya Jeshi la Polisi. ACT Wazalendo tunatoa wito kwa Rais Samia kuongeza wigo wa tume hiyo kwa kuhusisha wadau wengine ili kulifanya Jeshi la Polisi kuakisi matarajio na matamanio ya watanzania wanaowahudumia,” amesema Maharagande.

Naye Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa Chama cha Wananchi (CUF), Mhandisi Mohamed Ngulangwa, alipongeza hatua hiyo huku akitoa wito ukaguzi wa kina ufanyike kwa Jeshi la Polisi.

“Pamoja na pongezi kwa Rais, tunaendelea kutoa wito wa kulifanyia ukaguzi wa kina jeshi hili kwa ngazi zote ili hatimae kuhakikisha tunakuwa na jeshi bora. Matokeo ya ukaguzi huo yatumike kuboresha ufanisi, kudhibiti watumishi waovu, lakini pia kuboresha maslahi na mazingira ya kazi ya jeshi hilo,” alisema Mhandisi Ngulangwa na kuongeza:

“Tunautakia uongozi mpya wa jeshi la polisi utendaji uliotukuka unaozingatia weledi, uwajibikaji na unaoheshimu misingi ya haki za binadamu na utawala bora.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!