Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mufti: Sensa ni msingi mkuu wa maendeleo
Habari Mchanganyiko

Mufti: Sensa ni msingi mkuu wa maendeleo

Spread the love

MUFTI wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir, amesema sensa ni msingi mkubwa wa maenndeleo ya mtu na hivyo kutoa wito kwa waislamu wote kushiriki zoezi hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Sheikh Zubeir ameyasema hayo leo Jumapili tarehe 10 Julai, 2022, wakati akitoa mawaidha kwenye baraza la Eid Al Adha lililofanyika katika Msikiti wa Mfalme wa Morroco, Muhhamad wa sita jijini Dar es Salaam.

“Kama hakunasensaa hakuna maendeleo mahali  popote, mimi nitastaajabu watu wasiopende sensa wakati dunia nzima inafanya sensa,” amesema Sheikh Zubeir.

Ametolea mifano nchi ya Saudi Arabia “inafanya sensa muda ungeruhusu au ingekuwa natoa muhadhara ningeeleza muda iliyofanya sensa.  Masri  wanafanya sensa kama ukitaka Masheikh waende pale wameandika kuna maelefu hapa kama wewe, hiyo ni sensa,”

“Sheikh wa wapi unakataa sensa unawashinda hata masheikh wa Masri, unawashinda Masheik wa Saudia, kwamba una elimu kubwa kuwashinda.”

“Hapa nina maelezo mengi kuhusu sensa waislamu jitokezeni kuhesabiwa tarehe 23 kwasababu sensa ni maendeleo ya mtu mmoja mmoja hata wewe nyumbani kwako kama huna sensa utaishia maisha ya ajabu,” amesisitiza Zubeir.

Amesema Serikali inataka kujua ina watu wangapi ili ijue mahitaji yanayohitajika, “inataka kujua itatengeneza barabara kiasi gani mijini na vijijini, itajenga hospitali ngapi, shule ngapi, wanataka kuelewa, chakula kiasi gani, ajira, maji kiasi gani.

“Unataka sisi tufe kwa kupewa kidogo kumbe tuko wengi, vituo vya afya vichache kumbe tuko wengi, waalimu wangapi wanahitajika msingi hadi chuo kikuu, sensa hiyo.”

Sheikh Zubeir amesema anasimama sana kwenye suala hilo la sensa kutokana na miaka ya huko nyuma baadhi ya masheikh kupinga zoezi hilo.

“Nasimama sana katika suala la sensa kwasababu zamani kipindi cha Rais Jakaya Kikwete Masheikh walipinga na mimi nikasimama nikasema hapana, sensa ni jambo zuri,” amesema.

“Niwahimize Masheik wa mikoa wilaya, kata maimamu wawahimize waislamu kwenda kuhesabiwa na kuacha shughuli zao wakahesabiwe,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!