Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bajeti yashauri mambo saba deni la Taifa
Habari za Siasa

Kamati ya Bajeti yashauri mambo saba deni la Taifa

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Daniel Sillo
Spread the love

 

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imeshauri mambo saba kuhusu deni la taifa “pamoja na kwamba deni hilo ni himilivu.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)

Hadi mwezi Machi 2022, deni la Serikali lilikuwa ni Sh69.44 trilioni ukilinganisha na Deni la mwezi Machi 2021, la Sh64.46 trilioni Sawa na ongezeko la asilimia 7.73 (Sh4.98 trilioni).

Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya Bajeti leo Alhamisi tarehe 16 Juni 2022, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Daniel Sillo amesema wanaishauri Serikali kuangalia uwezekano wa kujipima uhimilivu wa deni kwa kutumia kiashiria cha makusanyo ya mapato ya ndani kwa ulipaji wa deni.

“Hii ni kwa sababu deni la Serikali hulipwa na makusanyo ya ndani na ni malipo ya lazima (first charge) katika matumizi ya Serikali,” amesema.

Kwa kuwa Tanzania ilipata The Debt Service Suspension Initiatives– DSSI toka benki ya Exim ya China (US$ 99.5 million) na French Development Agency (US$2.6 million), kamati imeishauri Serikali kulipa madeni haya mara tu muda wa kulipa utakapofika ili kuondoa tatizo la malimbikizo ya madeni

Pia imeishauri kukamilisha haraka mchakato wa kufanyiwa tathmini ya uwezo wa ukopaji na ulipaji (credit rating) ili kuiwezesha Serikali kupata mikopo yenye masharti nafuu na kwa urahisi

Mbali na hayo Kamati uimeshauri mikopo yenye masharti ya kibiashara ielekezwe katika miradi yenye sura ya kibiashara, kuboresha mikakati ya kukusanya kodi, kutafuta mikopo yenye masharti ya kati na izingatiwe kwamba gharama za mikopo ya biashara zitaongezeka kutokana na kuongezeka kwa riba za mikopo katika mataifa yaliyo endelea pamoja na mfumuko wa bei.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!