Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Tozo ya miamala kupunguzwa
Tangulizi

Tozo ya miamala kupunguzwa

Spread the love

 

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema Serikali itapunguza tozo ya muamala kutoka kiwango kisichozidi Sh. 7,000 hadi kiwango kisichozidi Sh. 4,000 . Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 14 Juni 2022 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali, kwa mwaka wa fedha wa 2022/23.

“Napendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa, kwa kupunguza tozo ya muamala kutoka kiwango kisichozidi shilingi 7,000 hadi kiwango kisichozidi shilingi 4,000 katika kila muamala wa kutuma au kutoa pesa,” amesema Dk. Mwigulu na kuongeza:

“Punguzo hili ni sawa na asilimia 43 ya kiwango cha sasa. Sambamba na hilo, napendekeza kuongeza wigo wa tozo hiyo ili kuhusisha miamala yote ya kielektroniki. Lengo la hatua hii ni kupunguza makali ya maisha kwa mtanzania hasa katika kipindi hiki cha changamoto kubwa ya kiuchumi na kuweka usawa katika utozaji wa tozo hiyo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!