Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kupunguza mrabaha kwenye dhahabu, makaa ya mawe
Habari za Siasa

Serikali kupunguza mrabaha kwenye dhahabu, makaa ya mawe

Madini ya dhahabu
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, inakusudia kupunguza viwango vya mrabaha wa madini ya dhahabu na makaa ya mawe, yanayozalishwa nchini, katika mwaka wa fedha wa 2022/23. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 14 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka 2022/23.

Dk. Nchemba amesema, wizara yake inapendekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, ili kupunguza kiwango cha kutoza marabaha kutoka asilimia sita hadi nne, kwa dhahabu inayouzwa kwenye vituo vya kusafisha madini.

https://www.youtube.com/watch?v=031HQcTN_qs

“Lengo la hatua hii ni kuhakikisha kuwa vituo vilivyoanzishwa nchini vinapata malighafi ya kutosha kwa ajili ya kusafisha na hatimaye kuongeza ajira na mapato ya Serikali,” amesema Dk. Mwigulu.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwigulu amesema, Serikali inakusudia kupunguza kiwango cha marabaha kutoka kwenye makaa ya mawe yanayotumika kama malighafi za kuzalisha nishati viwandani, kutoka asilimia tatu hadi moja.

“Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za uzalishaji viwandani, kuchochea uwekezaji zaidi na kukuza ajira,” amesema Dk. Mwigulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!