Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari Wizara ya Habari yapokea asilimia 53 fedha za maendeleo
HabariTangulizi

Wizara ya Habari yapokea asilimia 53 fedha za maendeleo

Nape Nnauye, Waziri wa Habari
Spread the love

 

HADI kufikia tarehe 30 Aprili, 2022 Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (Fungu 68) imepokea jumla ya Sh. bilioni 129.7 kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ambayo ni asilimia 53.7 ya fedha zilizotengwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo Ijumaa tarehe 20 Mei 2022 na Waziri wa Habari, Nape Nnauye, akiwasilisha makadiirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2022/23.

Katika Mwaka wa Fedha 2021/22 Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari iliidhinishiwa kutumia kiasi cha Sh. 246.3 bilioni.

Nape amesema kati ya fedha hizo Sh. 4.9 bilioni iliidhinishwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh. 241.3 iliidhinishwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

Aidha, ameongeza kuwa Idara ya Habari – MAELEZO na Taasisi za TBC na TSN zilikuwa zimetengewa bajeti ya jumla ya Shilingi 23.7 bilioni kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali.

Amesema kati ya fedha hizo Sh. 17.7 bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya awaida na Sh. 6 bilioni ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

Kwa upande wa bajeti ya Matumizi ya Kawaida Nape amesema hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2022 Wizara imepokea na kutumia jumla ya Sh. 6.9 bilioni sawa na asilimia 84 ya fedha zilizotengwa.

Amesema kati ya fedha za matumizi ya kawaida zilizopokelewa Sh. 2.2 bilioni ni za Mishahara na Sh. 4.6 bilioni ni Matumizi Mengineyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!