Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari Kigwangalla ataka mabadiliko mgawanyo wa ajira
HabariHabari Mchanganyiko

Kigwangalla ataka mabadiliko mgawanyo wa ajira

Spread the love

MBUNGE wa Nzega Vijijini, Dk. Hamisi Kigwangalla (CCM), ameishauri Serikali ibadili mfumo wa utoaji ajira za watumishi wa umma, akitaka iajiri watu kutoka maeneo yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Dk. Kigwangalla ametoa ushauri huo leo Alhamisi, tarehe 19 Mei 2022, akizungumza katika ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan, mkoani Tabora.

Mbunge huyo wa Nzega Vijijini, ametoa ushauri huo akizungumzia ajira zilizotangazwa na Serikali hivi karibuni, zaidi ya 10,000.

“Tunafahamu utaratibu wa kawaida watoto wataajiriwa central halafu watasambazwa kwenye maeneo yenye uhitaji nchi nzima. Sisi tunaomba kuwe na usawa kwenye kugawa nafasi za ajira wachaguliwe kutoka katika eneo wanalotoka katika majimbo yao,” amesema Dk. Kigwangalla.

Dk. Kigwangalla amesema “kama ambavyo mmetugawia pesa za barabara kwenye kila jimbo, basi hivyo hivyo na nafasi za ajira zigawanywe kwa usawa kutokana na vigezo mbalimbali ambavyo Serikali haitashindwa kuweka.”

Katika hatua nyingine, Dk. Kigwangalla ameiomba Serikali ikamilishe ujenzi wa miradi ya maendeleo, iliyoanza kujengwa jimboni mwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!