Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinana: Waliotajwa ripoti ya CAG wawajibishwe
Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Waliotajwa ripoti ya CAG wawajibishwe

Makamu Mwenyekiti wa chama tawala Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa chama tawala Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ameishauri Serikali inayoongozwa na chama hicho kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wale waliyotajwa kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Kinana ametoa ushauri huo leo Jumatano tarehe 27 Aprili 2022 ikiwa ni siku ya nne nay a mwisho ya ziara katika mikoa minne akianzia Pwani, Tanga, Kilimanjaro na kumalizia Arusha.

Ushauri huo kwa Serikali anaitoa kipindi ambacho Ripoti ya CAG Charles Kichere inayoishia 30 Juni 2021 iliyowasilishwa bungeni na Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni, imeonesha wizi na ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma.

Akizungumza kwenye mkutano wa ndani wa chama hicho mjini Arusha, Kinana amesema ni muhimu wote waliyotajwa kwenye ripoti ya CAG kuchukuliwa hatua.

“Wakati umefika kwa serikali kuchukua hatua kwa wahusika waliyotajwa. Ripoti ile inaonesha mambo ya hovyo. Si uzushi imefanywa kisayansi na kitaaluma imeandikwa,” amesema Kinana.

“Mimi nadhani ingekuwa vyema hatua ziwe zinachukuliwa papo kwa papo ili watu waogope kutumia fedha za umma,” amesema Kina a huku akishangliwa na wanachama wa chama hicho.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere

Kinana ambaye alikuwa anahitimisha ziara yake ya mikoa minne kukagua uhai wa chama, amesema pamoja na kwamba hana mamlaka ya kutoa amri kwa serikali lakini atamwambia Rais Samia juu ya ushauri huo.

“Kwa nafasi yangu nazungumza kwa niaba ya mwenyekiti wetu ambaye ni Rais kwamba wahusika wachukuliwe hatua,” amesema.

Kinana aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CCM amesema lazima kuwe na utaratibu wa kuwajibika mtu anapofanya kosa.

“Tujenge utamaduni wa kuwahi bila mtu akae pembeni apishe wengine. Kwani si kuna wengi wana uwezo hawana kazi! wakae pembeni waje wengine” amesema

“Kila ripoti ya CAG inapotolewa tukianzia na hii wale wanaotajwa wawajibike. Vyombo vya serikali vichukue hatua kwa yale yaliyotajwa mle ili fedha za wananchi zisichezewe,” amesema.

2 Comments

  • Nakubaliana na Komredi Kinana. Hatua lazima zichukuliwe. Lakini CCM si ndio inashika hatamu ya serikali? Mbona nyinyi ndio mna uwezo wa kuwachukulia hatua mafisadi na wezi? Unamtaka nani achukue hatua? Mwenyekiti wako si ndio mkuu wa taifa na jemadari mkuu?

  • Asante ndugu kinana nasi tinaomba hatua kali za kisheria zifanyike kwa vitendo na sio kwa maneno kama ilivyo kawaida yetu. Mwizi wa mali ya umma ni sawa na punguwani akilizake zimehama mali ya umma ambayo iinastiri nchi na family yake anaitafuna and kuimeza anatakiwa amalizike kabla ya mali haijamalizika

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!