Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanaosema miradi haitaendelezwa wana upeo mdogo: Samia
Habari za Siasa

Wanaosema miradi haitaendelezwa wana upeo mdogo: Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema watu wanaofikiri kwamba miadi iliyoachwa na mtangulizi wake haitaendelezwa wana upeo mdogo wa kufikiri. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 23 Machi 2022, akizundua nyumba za Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.

Amesema waliokuwa wanasema hivyo hawakuwa hata na sababu na kubainisha kuwa hakuna sababu ya miradi kutoendelea kwasababu imeagizwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Serikali zote zinazoongoza Tanzania ni za Chama Cha Mapinduzi awamu moja ikiondoka awamu ya pili inashika Serikali… kwahiyo wanaposema kwamba miradi haitatekelezwa nadhani upeo wao wa kufikiri ni mdogo sana,” amesema na kuongeza;

“Hata miradi hii ilivyoanzishwa awamu ya tano mimi nilikuwa Makamu wa Rais kwahiyo ni sehemu ya miradi hiyo kuanza kwake na kutekelezwa kwake.

“Lakini kwa kunitazama sura na kusema asingeweza kuendeleza hii miradi haikuwa busara, lakini tuwaombee nasi tujiombee Mungu atupe nguvu na busara zaidi miradi hii iendelee kwa maendeleo ya nchi yetu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!