Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko LHRC yaunga mkono upatikanaji katiba mpya baada ya 2025
Habari Mchanganyiko

LHRC yaunga mkono upatikanaji katiba mpya baada ya 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga
Spread the love

 

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema kinaunga mkono mapendekezo ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama vya Siasa, ya mchakato wa ulatikanaji katiba mpya kuanza baada ya 2025. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 22 Machi 2022, jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga.

Henga amesema, 2025 sio mbali kwa kuanza mchakato huo, huku akipongeza hatua ya Rais Samia kuruhusu marekebisho hayo kufanyika kitendo ambacho kilipingwa na mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.

“Lengo ni mchakato wa katiba ufufuliwe bila kujali muda, hapo nyuma hatukujua unaanza lini lakini sasa hivi umefufuliwa. 2025 sio mbali unaweza kuwa muda mzuri,” amesema Henga.

Alipoulizwa kama LHRC ina imani na kikosi kazi hicho, Henga amesema “Tunaimani nacho sababu kilipoteuliwa kimeteuliwa kwa kuchukua wajumbe kutoka kada tofauti. Hatujaona mrengo wa wanasiasa, hakijaegemea mrengo fulani. Mwenyekiti wake ni mwanataaluma.”

Kikosi kazi hicho kiliundwa mwishoni mwa 2021, kwa ajili ya kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na washiriki wa mkutano wa wadau wa vyama vya siasa, uliofanyika jijini Dodoma Desemba mwaka jana, kwa ajili uboreshaji sheria na katiba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa aanika mafanikio ya TMA

Spread the loveSHUGHULI za Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), zimeimarika...

error: Content is protected !!