Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Wanamichezo Urusi, Belarus wapigwa marufuku Paralimpiki
Michezo

Wanamichezo Urusi, Belarus wapigwa marufuku Paralimpiki

Spread the love

WANAMICHEZO wote waliotarajia kushiriki michezo ya Paralimpiki msimu wa baridi, inayotarajiwa kuanza rasmi kesho Beijing nchini China, wamepigwa marufuku. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Taarifa iliyotolewa na Kamati ya Kimataifa ya Paralimpiki (IPC) leo tarehe 3 Machi, 2022, imesema hali ni mbaya katika kijiji inakofanyika michezo hiyo na imekuwa vigumu kuhakikisha usalama wa wanamichezo hao unaendelea kuwepo.

Uamuzi wa awali wa IPC kuruhusu wanamichezo 71 wa Urusi na 12 wa Belarus kushiriki bila kuonyesha upande wowote, umekosolewa vikali.

“Tunaamini kabisa kuwa michezo na masuala ya kisiasa hayapaswi kabisa kuchanganywa,” amesema Rais wa IPC katika taarifa yake hii leo na kuongeza;

“Hata hivyo, ni bahati mbaya kwamba vita vimeingia katika hii michezo na nyuma ya pazia Serikali zimekuwa na ushawishi katika tukio letu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!