Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Wanamichezo Urusi, Belarus wapigwa marufuku Paralimpiki
Michezo

Wanamichezo Urusi, Belarus wapigwa marufuku Paralimpiki

Spread the love

WANAMICHEZO wote waliotarajia kushiriki michezo ya Paralimpiki msimu wa baridi, inayotarajiwa kuanza rasmi kesho Beijing nchini China, wamepigwa marufuku. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Taarifa iliyotolewa na Kamati ya Kimataifa ya Paralimpiki (IPC) leo tarehe 3 Machi, 2022, imesema hali ni mbaya katika kijiji inakofanyika michezo hiyo na imekuwa vigumu kuhakikisha usalama wa wanamichezo hao unaendelea kuwepo.

Uamuzi wa awali wa IPC kuruhusu wanamichezo 71 wa Urusi na 12 wa Belarus kushiriki bila kuonyesha upande wowote, umekosolewa vikali.

“Tunaamini kabisa kuwa michezo na masuala ya kisiasa hayapaswi kabisa kuchanganywa,” amesema Rais wa IPC katika taarifa yake hii leo na kuongeza;

“Hata hivyo, ni bahati mbaya kwamba vita vimeingia katika hii michezo na nyuma ya pazia Serikali zimekuwa na ushawishi katika tukio letu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!