Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Vita Urusi-Ukraine: Tanzania yatangaza neema bei ya mafuta
Habari Mchanganyiko

Vita Urusi-Ukraine: Tanzania yatangaza neema bei ya mafuta

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kuondoa tozo ya Sh.100 kwa lita ya mafuta ya Dizeli, Taa na Petroli zinazopaswa kulipwa na watumiaji wa mafuta kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia tarehe 2 Machi hadi Mei 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo Jumatatu tarehe 28 Februari 2022 na Wizara ya Nishati kutokana na kupanda kwa bidhaa hizo katika soko la dunia kutokana na mbalimbali ikiwemo vita vya Urusi na Ukraine.

Taarifa hiyo imeeleza kwamba, Serikali itaendelea kutathimini mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia.

 

“Pamoja na kwamba, uamuzi huu utaipunguzia Serikali mapato ya Sh.30 bilioni kwa mwezi, Serikali imeona ni muhimu kuwalinda wananchi wake dhidi ya athari za mabadiliko ya bei za mafuta ulimwenguni,” imeeleza taarifa hiyo

Katika taarifa hiyo, imefafanua kwamba, Waziri wa Nishati, January Makamba ameidhinisha na kusaini marekebisho ya kanuni inayohusika na tozo hiyo ili kutimiza uamuzi huo wa Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!