Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, wenzake wanyimwa chakula miezi 5
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, wenzake wanyimwa chakula miezi 5

Spread the love

 

KIONGOZI wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania-Chadema, Freeman Mbowe ameibuka malalamiko mahakamani ya kunyimwa chakula kwa zaidi ya miezi mitano kila wanapokwenda kusikiliza kesi yao ya ugaidi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mbowe kwa niaba ya wenzake watatu, amedai hayo leo Jumatatu, tarehe 14 Februari 2022, Mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam mbele ya Jaji Joachim Tiganga.

“Sisi watuhumiwa tumenyiwma haki ya kula zaidi ya miezi mitano, tulipokuja kwenye mahakama yako, tumekosa haki ya kula kwa miezi mitano. Mheshimiwa jaji mnapokuwa mnaahirisha kesi kupata chakula cha mchana, sisi tumekuwa tukikosa chakula hata soda, sasa tunataka kujua kuna utaribu wa hivyo au Jeshi la Magereza kutupatia chakula au familia zetu kama wanavyotupatia,” amedai Mbowe

Mwenyekiti huyo wa Chadema amesema, tulikuwa hatuli siku zote, mwanzoni tuliambiwa kama ni kula mchukue chakula kutoka gerezani mje nacho mahakani, sisi tuaishi jela hatuna friji kuhifahdi chakula, kwa hiyo tuletewe chakula Jumamosi tuhifadhi tukaona tutakula sumu. Tunaenda kukesha katika magereza bila chakula chochote hata soda hatupati.

Mara baada ya Mbowe kutoa malalamiko hayo, Jaji Tiganga akawauliza mawakili wa utetezi, “mmekuwa mkitoa uwakilishi gani mahakamani kama wateja wenu wanatuambia hawajala kwa miezi mitano? Nyie mko hapa mlikuwa mnawakilisha, hamkumuona kama ni haki ya wateja wenu?”

Baada ya Jaji Joachim Tiganga, kuhoji hayo, kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi, Peter Kibatala akasimama kujibu akisema “tulifahamu ni tatizo awali, tukawasiliana na liaison officer wa magereza, akatuahidi atashughulikia.”

Jaji Tiganga ameahirisha kwa muda kesi hii na kuwaita mawakili wa pande zote mbili kujadiliana kuhusu suala hilo.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!